“WATANZANIA TUJITATHMINI NA SIASA ZETU”

Saturday, August 10, 2013



Katika juhudi zetu za kuleta maendeleo ya vijana, jamii na taifa kwa ujumla; na kugusa mahitaji  muhimu , ni lazima kukumbuka kwamba binadamu ni wa muhimu zaidi ya mahitaji yake, na muhimu zaidi katika hili ni kuifanya jamii ijiletee maendeleo yake inayoyahitaji. Hivyo wadau wa maendeleo, serikali ikiwa mstali wa mbele ni kuweka mazingira rafiki kwa maendeleo. Mazingira haya ni yale halisi mfano: rasilimali na mazingira ya nadharia mfano: mazingira ya kijamii, kisiasa, kichumi na kitamaduni.
Ni jambo la kusikitisha sana kwa siasa za Tanzania ya leo, kwani zinakampeni ya kulenga mahitaji ya watu zaidi kuliko watu wenyewe. Vijana na watanzania wote kwa ujumla tuweni welevu na wenye busara juu ya mustakabali mzima wa siasa na wanasiasa. Napenda kutoa wito kwa watanzania wote hasa vijana, tuwe na tafakari ya kina na kuchukua hatua. Nipo kwenye mkakati wa kuwaandikia watanzania kijarida chenye kichwa cha habari “WATANZANIA TUJITATHMINI NA SIASA ZETU” humo nitazungumza mengi juu ya mwenendo wa siasa ya leo na madhara yatokanayo. Alisema Bw. Japheth M. Kurwa-Mkurugenzi wa TYPs-ASSOCIATION katika ofisi za Asasi hiyo ya maendeleo ya Vijana zilizoko ndani ya kituo cha Matumaini katika Vijana-Manispaa ya Musoma, tarehe 08/08/2013
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger