AJIRA: VIJANA AMBAO HAWAKUBAHATIKA KUENDELEA NA MASOMO.

Friday, November 21, 2014




Kundi hili ni kundi linalojumuisha vijana wengi zaidi kuliko lile la vijana wasomi. Vijana wengi walioko katika kundi hili ni wale walioko katika ajira zisizo lasmi kama vile; uvuvi, kilimo, kubeba mizigo, ufugaji, machinga, garage, udereva wa magari na pikipiki (Bodaboda), ulinzi, vibarua vya ujenzi, vibarua katika sekta ya madini, migahawa/ vibanda vya lishe na kuchoma chips, saloon, uselemala, vibarua viwandani n.k
1.   Tafsiri Baadhi ya Maneno
Ajira: Ni shughuli yoyote halali (rasmi au isiyo rasmi), inayomwezesha mwananchi kujipatia riziki, mahitaji na kipato cha kuendesha maisha yake, ya familia na pengine kuchangia katika pato la eneo alipo au Taifa.
Kutokuwa na ajira: Ni hali ya kukosa kazi kabisa au nguvukazi iliyopo kutotumika kuzalisha mali au kutoa huduma.
 Kijana: Zipo tafsiri aina mbili;
i)    Kimataifa; Kijana ni mtu mwenye umri wa miaka 15 hadi 24
ii)   Kwa Tanzania ni miaka 15 hadi 35
Sekta isiyo rasmi: Hii ni sekta ambayo si ya shambani wala ofisini, ya kiwango cha chini na ya kujiajiri   inayotumia mtaji na teknolojia ndogo.
Fursa: Ni shughuli za kiuchumi na kijamii au za uzalishaji mali au huduma ambazo hutekelezwa na mtu na kuweza kumpatia kipato halali.

2.   Fursa ya Uvuvi na Uzaji wa Samaki-Kisiwani Lukuba
Sekta ya Uvuvi ni moja ya sekta iliyoajiri vijana wengi hapa Tanzania, Kisiwa cha lukuba ni moja ya Visiwa vilivyoko mkoani Mara chenye fursa kubwa ya ajira ya kujiajiri.
Kisiwa hiki kinatoa fursa nyingi za ajira ya kujiajiri kwa vijana hususani wale ambao hawakubahatika kwendelea na masomo. Fursa za ajira ni uvuvi unaoambatana na usafirishaji, uchakataji, uchuuzi wa samaki na uzalishaji viwandani, ujenzi wa mitumbwi/boti za uvuvi.
Kisiwa hiki kinategemea shughuli ya uvuvi na uuzaji wa samaki hususani samaki aina ya Dagaa na Sangara (Nile perch). Uvuvi katika kisiwa hiki unatoa mchango mkubwa katika kuinua kiwango cha maisha ya vijana hawa, wananchi wa Musoma na nchi kwa ujumla. Hata hivyo, fursa bado ni kubwa kwa wawekezaji wengi kuwekeza katika eneo hili.
Serikali inatakiwa kuongeza juhudi za makusudi kuhakikisha uendelevu wa raslimali ya uvuvi ambayo ni msaada mkubwa kwa taifa. Aidha inatakiwa kuliangalia eneo hili kwa makini ili kuwawezesha vijana hususani kundi hili ambalo halikubahatika kuendelea na masomo yao.

3.   Changamoto ya Jumla Kuhusu Ajira ya Vijana ambao Hawakubahatika Kuendelea na Masomo.
Kundi hili ni kundi linalojumuisha vijana wengi zaidi kuliko lile la vijana wasomi, kwa mtazamo wa haraka kundi hili la vijana ni kama limesahulika.; changamoto zinazolikabili kundi hili ni pamoja na:-
·         Hali ya kutokuwa na fursa ya kushiriki katika uchumi inayosababishwa na uwezo mdogo katika mitaji, ukosefu wa ujuzi na uzoefu wa biashara, pamoja na matatizo yanayohusiana na kutokopesheka.
·         Hali ya kutopata fursa ya kushiriki katika fursa za kiuchumi katika mfumo rasmi
·         Kutopokelewa na jamii katika mtazamo chanya; kunakoleta tafasili kandamizi kwao kama vile tafasiri ya wahuni na watu waliofeli maisha, tafasili ambayo hupelekea vijana hao kuwa hivyo.
·         Uhusiano mdogo wa kundi hili na sekta rasmi, taasisi binafsi na za umma; na Serikali kwa ujumla

4.   Nini Kifanyike
Wadau wote wa maendeleo ya vijana (serikali, jamii, sekta binafsi, Asasi za kijamii, familia na vijana wenyewe) kuwa karibu sana na kundi hili kama walezi na walimu; na kutekeleza wajibu huu ipasavyo

Vijana kuchangamkia fursa na kuzitumia ipasavyo katika kuwekeza na kuzalisha (Saving and Production). Ogopeni semi kama vile: Tumia pesa ikuzoee, elfu moja haijengi, raha jipe mwenyewe, kula ujana maisha yenyewe mafupi n.k

Maeneo haya yenye kuwaajiri vijana walioko katika kundi hili, yakipewa kipaumbile na kutengenezwa kuwa mazingira rafiki ya kujiajiri yatapunguza kwa kiasi kikubwa kero ya ajira kwa vijana na taifa kwa ujumla.

By: Mr. Japheth M. Kurwa
Falsafa yangu ni:- “JUHUDI ZISIZOKOMA KATIKA KUJIFUNZA NA KUFANYA KAZI”

Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger