HAKI YA KUISHI MATATANI KWA WANAWAKE MKOANI MARA

Sunday, February 2, 2014




Simanzi na majozi vimeendelea kuikumba jamii ya mkoani Mara baada ya kuzuka Mauaji ya kikatili ya kuchinja vichwa kwa wanawake, kunyongwa na hata kuondolewa sehemu zao za siri ikiwa ni pamoja na kutobolewa macho kuendelea kushamili na kuifanya Haki ya Kusishi kubaki kuwa kitendawili kwa wanawake mkoani Mara hususani wilaya ya Butiama na Musoma. Mauji haya tangu kuzuka yapata ni mwaka mmoja sasa (tangu 2013) na ufumbuzi wake ni sitofahamu.
Mama mmoja kwa jina Nyasatu Paulo mwenye umri wa miaka 24, mkazi wa kijiji cha Kigera Etuma, Kata ya Nyakatende, Tarafa ya Nyanja, Wilayani Butiama-Mara, alikutwa mauti shambani kwake kwa kifo cha kunyongwa shingo na kisha kifukiwa kwa udongo wa matuta kama mzoga. Marehemu alipotea siku moja kabla (tarehe 30/01/2014 Alihamisi) ya kupatikana mashambani akiwa mauti (tarehe 31/01/2014 Ijumaa). Marehemu ameacha familia ya mume na watoto 3, mdogo ( mtoto wa tatu) akiwa mwenye umri wa miezi 8.
Wanainchi wenyeji wa maeneo ambamo mauaji haya hutokea wanabaini kuwa mauji haya yanatokana na sababu kuu mbili:1. Imani za kishirikina, na ya 2. Visasi. Eidha walibainisha kuwa Haki ya Usawa kwa wanawake pia imekuwa ndoana kwa wale wanaodhubutu kuisimamia na kuidai hususani kumiliki au kurithi rasilimali mfano ardhi, ng’ombe na nyumba.
Wanainchi wameendelea kuitupia serikali lawama kuwa haijaamua kutokomeza mauaji haya ya kikatili kwa wanawake yanayoendelea mkoani Mara. “Kama wanyamapori wanakufa na Serikali inaanzisha Oparesheni Tokomeza kuzuia mauaji ya wanyamapori/Majangiri, Je binadamu si rasilimali ya Taifa, mpaka ione haja ya kuwepo na Oparesheni ya kutokomeza mauaji haya…?, Ni ajabu serikali yetu kuliacha swala hili kwa sehemu kubwa mikononi mwa wanainchi!” Alisema Mkazi wa Kijiji cha Kigera Etuma kwa Uchungu.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger