VIJANA KUKUTANA NA FURSA ZA MAENDELEO-MUSOMA

Sunday, August 18, 2013





Pichani ni viongozi wa vikundi vya maendeleo ya vijana (vikundi 31) kutoka wilaya za Butiama na Musoma wakiwa na maafisa wa serikali na Asasi za kiraia katika picha ya pamoja ndani ya viwanja vya Kituo cha Matumaini katika Vijana-Manispaa ya Musoma


Maafisa hao ni pamoja na: Ndugu Adolfu Kami wa kwanza kushoto waliosimama mstari wa kwanza, afisa maendeleo ya vijana manispaa ya Musoma, ndugu Masatu Rugee, afisa michezo na utamaduni halimashauli ya wilaya ya Musoma, Afisa utawala na Fedha Ndugu Robert Moro, wa Shirika la Kutetea Haki za Wanawake na Watoto (ABC FOUNDATION); na Ndugu George Muyabi mratibu wa Mara Development Forum (MDF), pamoja na afisa mmoja wa CHODAWU na Idara ya Kazi na Ajira-Musoma
Asasi iliwakutanisha viongozi wa vikundi vya maendeleo ya vijana (vikundi 31) na maafisa hao kwa lengo la vijana hao kutambua fursa na wajibu wao ili waweze kunufaika na fursa zilizo katika ofsi za idara hizo za serikali 

“Kila kijana ni muhimu kutambua haki na wajibu wake; kila kijana ana haki na wajibu wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo yake bifsi, ya jamii pamoja na taifa kwa ujumla. Na kwa mantiki hii serikali, Asasi za kiraia, na jamii ni lazima kuhakikisha kuwa zinaweka mazingira rafiki (mazuri) kwa maendeleo yao na kushiriki kikamilifu katika Nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni”. Alisema Mkurugenzi wa Asasi ya Maendeleo ya vijana (TYPs-ASSOCIATION) Bwn. Japheth M. Kurwa
“Ili vijana waweze kunufaika na fursa za maendeleo ikiwemo mikopo itolewayo na serikali ni lazima wakizi vigezo stahili ambavyo ni pamoja na: usajiri angalau kwa ngazi ya Halmashauri, wawe na miradi na iwe halisi, miradi hiyo iwe rafiki wa mazingira, iwe na uwezo wa kupunguza umasiki, uelewa wa kikundi juu ya miradi hiyo, uwezekano wa mradi kulipa mkopo ndani ya miaka miwili, uwiano wa mkopo na mradi wenyewe, na upatikanaji wa soko la mazao ya miradi yao. Mikopo hii inalenga maendeleo ya vijana kwenye miradi hivyo ni muhimu kutambua kuna wajibu wa kufanya ili kunufaika na mikopo hiyo”. Alisema Ngudu Adolfu Kami, Afisa maendeleo ya vijana-Manispaa ya Musoma

“Kwa vijana wasio katika vikundi yya maendeleo, watengeneze vikundi ili kukizi vigezo vya kunufaika na fursa zinazokuja moja kwa moja kwenye vikundi na sio kwa mmoja mmoja. Na vikundi vyote vya maendeleo ya vijana viwe na njozi ya kujitengenezea fursa za ajira ili kupunguza umasikini uliokithiri. Vikundi ni lazima vijenge tabia ya uzalishaji na uwekezaji ili kuzalisha mitaji kwani vijana wengi ni wazuri kwa uzalishaji na matumizi hii haitawasaidia. Pia ni wakati sasa vikundi wa kuwa wanachama kwenye SACCOS ya Vijana na SACCOS nyingine ili viweze kupata mikopo ya mitaji kwa riba nafuu”. Alisema Ngugu Masatu Rugee, Afsa michezo na utamaduni Halimashauri ya wilaya ya Musoma.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger