SERA YA TAIFA YA MAENDELEO YA VIJANA

Wednesday, July 24, 2013


SERA YA TAIFA YA MAENDELEO YA VIJANA
Sera hii iliandaliwa kwa ajili ya kusimamia maslahi ya kijana, ambayo serikali iliandaa mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007
Sera ya taifa ya maendeleo ya vijana ya 2007 inalenga masuala ya maendeleo ya vijana ambayo ni pamoja na: uwezeshaji wa kiuchumi, mazingira, VVU na Ukimwi, jinsia, sanaa na utamaduni, michezo afya ya uzazi kwa vijana na masuala ya maisha ya familia.
LENGO LA SERA
  • Kuhakikisha taifa linakuwa na vijana wenye uwezo, wenye ari ya kutosha , wawajibikaji na wanaoshiriki kikamilifu katika Nyanja zote za kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa maendeleo ya jamii.
  • Kuweka mazingira yanayowezesha kujenga uwezo wa vijana na kukuza nafasi za ajira na kupata huduma ya hifadhi ya jamii
Kwa kifupi lengo ni kuwajengea uwezo, kuwawezesha na kuwaongoza vijana na wadau wenginekatika utekelezaji wa masuala ya maendeleo ya vijana
Sera ya taifa ya vijana imeandaliwa ili sisi vijana wa kike na wa kiumetuendelee kuleta msukumo wawa kuleta mageuzi ya kijamii, kiuchumi na kisiasa katika eneo lenye mabadiliko ya haraka duniani.
Maendeleo yetu ya kijamii yanategemea, pamoja na vitu vingine, ni kwa jinsi gani vijana tunahusika katika kujenga maisha ya baadaye. Hivyo ni kwa sababu hii sera inatuandaa kuwa viongozi, watoa uamuzi, wajasiriamali, wazazi na walezi kwa sababu tuna nafasi muhimu katika maendeleo ya jamii na uchumi wa taifa letu.
Sera ya taifa ya vijana imetoa maelekezo kwa vijana, washirikiane na wadau wengine katika masuala ya maendeleo yetu. Ila sera ni muongozo tu, utekelezaji wake ndio utakao tuwezesha kuvuna matunda ya sera hii nzuri .hatuna budi kuijua na kusimamia utekelezaji wake kwenye Nyanja mbalimbali kuanzia kwenye maeneo tunayoishi hadi serikali kuu
Wadau wote tushirikiane katika kutekeleza sere hii, hakika tutatengeneza vijana watakaolipeleka taifa hili mbele kimaendeleo (fema, APRIL-JUNE 2013.ONE DAY YES!, Youth POWER!, Zungumza na Mwanafunzi. Uk wa 2)
Share this article :

2 comments:

  1. You actually make it seem so easy with your presentation but I find this topic to
    be really something that I think I would never understand. It seems
    too complicated and extremely broad for me.
    I'm looking forward for your next post, I'll try to get the hang
    of it!

    ReplyDelete
  2. weka document ya sera ya vijana humu tuweze kuipakua, swahili version

    ReplyDelete

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger