ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI YATOLEWA KWA VIJANA WA MIAKA 15-25 MANISPAA YA MUSOMA

Sunday, August 18, 2013




 TANZANIA YOUTH POTENTIALS ASSOCIATION (TPYs-ASSOCIATION), Asasi ya maendeleo ya vijana yenye makao yake katika manispaa ya Musoma imewakutanisha vijana wapatao 87 na Shilika la Swiss Contact lenye makao makuu yake inchini Swaziland chini ya mradi wake wa U-Learn Program unaowalenga vijana wenye umri kati ya miaka 15-25. Malengo ya mradi huo ni vijana kuweza kujiajiri, hivyo hutoa elimu na  mafunzo ya ufundi kwa vijana.

“Naamini maendeleo ya vijana yataletwa na vijana wenyewe, wakishikwa mkono na wadau wa maendeleo yao, akiwemo mdau mkuu ambaye ni serikali, lakini vijana hatuna budi kuijua Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana na kusimamia utekelezaji wake kwenye Nyanja mbalimbali kuanzia kwenye maeneo tunayoishi hadi serikali kuu. Kwa hali ya kutokuwa na ufadhiri tunafanya kazi kwa kujituma, nidhamu, kujitoa kwa wito; na kujitahidi kuwakutanisha vijana na fursa mbalimbali za maendeleo yao wakiwemo wadau mbalimbali wa maendeleo ya vijana”. Alisema Bwana Japheth M. Kurwa-Mkurugenziwa Asasi
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger