MAUAJI YA KIKATILI DHIDI YA WANAWAKE KUENDELEA MKOANI MARA

Monday, April 14, 2014



Kulia juu ni picha ya mwili wa marehemu Nyamata Gwanumbu Monda Nyamsha, na ya pili ni maafisa wa polisi wakishusha mwili wa mareheu nyumbani kwao Kiemba Nyakatende.

Mama mmoja aliyefahamika kwa majina ya Nyamata Gwanumbu Monda Nyamsha, mwenye umri wa miaka iliyokadiriwa 38, watoto 5. Mkazi wa Mkoa: Mara, Wilaya: Butiama, Kata: Nyakatende, Kijiji: Kiemba. Tarehe 10 April, 2014 Saa 3 Asubuhi alikutwa shambani kwake akiwa mauti na amezikwa kwa kufukiwa kwa udongo chini ya kichaka kilichoko shambani kwake, hata hivyo marehemu alikutwa ana jereha la kupigwa kichwani eneo la kisogoni.


Kisa Mkasa
Marehemu asubuhi aliwahi kuamka na kuelekea shambani kwake kuchimba viazi huku akiwa amewaachia watoto wake maagizo ya kuja saa 3 asubuhi shambani hapo kumpokea viazi atakavyokuwa amechimba. Mda huo ulipofika watoto wa marehemu walikwenda shambani kufuata viazi kama marehemu mama yao alivyokuwa amewaambia.  Walipofika shambani hawakumuona marehemu mama yao ndipo walianza kuita mama mama……, ghafla walimuona mtu (mwanamume) akitoka kichakani akiwa uchi kama alivyozaliwa akiwa na panga mkononi, walikimbia wakipiga kelele.  Ndipo wananchi walipojitokeza kujua kulikoni. Katika zoezi la kumtafuta mama huyo ndipo alipokutwa kichakani hapo akiwa ameuwawa.
Kwa mujibu wa Mhe. Diwani wa kata ya Nyakatende Ndg.Kasonyi mauaji hayo ni mauaji ya nne(4) tangu mauaji hayo yaanze kuzuka wilani Butiama, Mugango mauaji mara mbili (2), yakiongozwa na Nyegina mauaji mara nane (8)

Tarehe 22/03/2014 saa 2 Asubuhi  yalitokea mauaji mengine pia ya mama aliyefahamika kwa majina ya Yasinta Kate Matiku kwa kabila Mkwaya, miaka 34, na familiya ya watoto 2. Mkazi wa Kijiji cha Kamguruki, Kata ya Nyakatende, Tarafa ya Nyanja, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara.

Kisa Mkasa
Asubuhi ya saa 2 marehemu aliondoka nyumbani kwenda kununua vitumbua gengeni(Center), ndiko alipokutwa na mauaji hayo. Mwili wake ulikuwa unajeraha kupigwa na kitu chenye incha kali, kisha kumwagiwa maji ya moto sehemu za mapajani, mgongoni na mbavuni, mkanda wa suruali shingoni na ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo vyake vya siri (maalufu kwa jina la Memory card)
Ukiwa mzalendo na mpenda Amani unashauri nini kifanyike………………………….?, Toa maoni yako ili kutokomeza mauaji haya yanayoendelea.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger