Karibu Musoma Information Center kwa huduma zifuatazo:- 1) Kwa kutengenezewa design mbalimbali kama za Business card, Vipeperushi, mabango mbalimbali, kadi za Harusi za kisasa zaidi, kadi za mialiko mbalimbali, Vitambulisho vya wanafunzi wa sekondari na katika kampuni mbalimbali ( ID cards) na kadi nyinginezo zenye design ya kuvutia. 2) Kutengenezewa mabango ( Posters) mbalimbali zinazohusu biashara ya mhusika au bidhaa mbalimbali. 3) Kutengenezewa nembo ( LOGO) za kuhusiana kampuni au biashara yako. 4) Tunatengeneza tovuti ( Websites ) zenye kiwango ambacho huwezi amini kama zinatengenezwa musoma, kwa bei nafuu ambayo huwezi ipata kwingine isipo kuwa kwetu. 5) Mwisho tunatoa ushauri na elimu kuhusiana na maswala ya computer.5) Sisi ni watengenezaji wa blog zinazokaa mfumo wa website. kama hii unayoiona.

Welcome to TYPS - ASSOCIATION

Welcome to TYPS - ASSOCIATION

Welcome

A Letter from the Executive Director

Dear All,

As Executive Director it is my pressure to welcome you to TANZANIA YOUTH POTENTIALS ASSOCIATION (TYPs-ASSOCIATION)-a growing youth-led Organization with it’s headquarter in Musoma that operates through legal registration number 00NGO/00006304 under the ACT of 2002 in Tanzania. The focus of the organization is to utilize youth’s potentials for their own development, community and state development at large. It also intends to strengthen regional and international interventions towards protection and promotion of the human rights especially to children, youth and women. It works with networking with other partners/ stakeholders and beneficiaries.

The Organization has the mission of striving and inheriting youth and other community groups with various technical capacities eligible to make them be engines for socio-economic growth for individual benefits, societies and the national at large as such to see a community in which women’s and children’s rights are observed and respected by executing mobilization projects eligible to bring positive changes to community through action and participation in collaboration with community and other stakeholders to prevent Gender Based Violence (GBV).

However the organization is dedicated to develop dynamic and entrepreneurial youths who will engage and realize their full potential and that of their community, their country and the world at large and advocating The National Youth Development Policy

The Secretariat , the Board of Directors and the Annual General Meeting of TYPs-ASSOCIATION eagerly anticipate your arrival and contribution to its future, and welcome you to discover youth development experience that promotes your Personal and intellectual growth

Welcome to TYPs-ASSOCIATION,
Mr. Japheth M. Kurwa
Executive Director


TWAWEZA KUONDOA UKATILI WA AINA ZOTE DHIDI YA WANAWAKE

Monday, August 19, 2013


Pichani ni wanaharakati wa haki za binadamu mkoani Mara. Kushoto wameshikilia mabango ya kupinga ukatili wa kijinsia/ nyumbani na kulia ni wananchi wa kijiji cha Bisumwa, kilichopo Kata ya Bisumwa, wilaya ya Butiama mkoani Mara wakiangalia sinema ya ukatili kijinsia/ nyumbani. Tukio hili lilifanyika jumapili ya tarehe 28/07/2013 kijijini hapo. Huu ni mdaharo wa wazi uliendeshwa chini ya Kampeni ya tunaweza yenye ujumbe “ Jamii kutoona ukatili wa kijinsia ni sehemu ya maisha”

ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI YATOLEWA KWA VIJANA WA MIAKA 15-25 MANISPAA YA MUSOMA

Sunday, August 18, 2013




 TANZANIA YOUTH POTENTIALS ASSOCIATION (TPYs-ASSOCIATION), Asasi ya maendeleo ya vijana yenye makao yake katika manispaa ya Musoma imewakutanisha vijana wapatao 87 na Shilika la Swiss Contact lenye makao makuu yake inchini Swaziland chini ya mradi wake wa U-Learn Program unaowalenga vijana wenye umri kati ya miaka 15-25. Malengo ya mradi huo ni vijana kuweza kujiajiri, hivyo hutoa elimu na  mafunzo ya ufundi kwa vijana.

“Naamini maendeleo ya vijana yataletwa na vijana wenyewe, wakishikwa mkono na wadau wa maendeleo yao, akiwemo mdau mkuu ambaye ni serikali, lakini vijana hatuna budi kuijua Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana na kusimamia utekelezaji wake kwenye Nyanja mbalimbali kuanzia kwenye maeneo tunayoishi hadi serikali kuu. Kwa hali ya kutokuwa na ufadhiri tunafanya kazi kwa kujituma, nidhamu, kujitoa kwa wito; na kujitahidi kuwakutanisha vijana na fursa mbalimbali za maendeleo yao wakiwemo wadau mbalimbali wa maendeleo ya vijana”. Alisema Bwana Japheth M. Kurwa-Mkurugenziwa Asasi

VIKUNDI VYA SANAA YA UIGIZAJI KUJENGEWA UWEZO-MUSOMA



Pichani-kulia (picha ya mkono wa kushoto mwenye) t-shirt ni M/Kiti wa kikundi cha Nyota Sanaa Group ndugu Majura Majura akicheza mchezo wa kuigiza na timu ya MINIBUZZ-Toa hoja!. Kwenye soko la Nyakato-Musoma. Katika ziara yao mjini Musoma. Kikundi hiki ni baadhi ya vikundi vya maendeleo ya vijana vinavyijishughulisha na sanaa ya uigizaji walivyovitembelea na kuigiza nao kwa kuwajengea uwezo. TYPS-ASSOCIATION (ASASI YA MAENDELEO YA VIJANA) inajumla ya vukundi 31 vya maendeleo ya vijana

TYPs-ASSOCIATION KUENDESHA MAFUNZO YA UJASILIAMALI



Pichani ni kikundi cha maendeleo ya vijana kilichopo kijiji cha Ryamisanga, Kata ya Bwiregi, Wilayani Butiama-Mara. Aliyesimama, mwenye t-shirt ya njano ni Mwl. Magta Nyangore (Mwezeshaji wa elimu ya ujasiliamali kwa program ya “Kazi Nje Nje” ya ILO). Mafunzo hayo yalitolewa kwa ushirikiano na Asasi ya TYPs-ASSOCIATION kwa mkakati wake wa kutekeleza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana.

WiLDAF KUONGEZA UWEZO KWA MAKUNDI YA WANAWAKE NA ASASI ZA KUTETEA HAKI ZA WANAWAKE-MUSOMA



Warsha ya Kuongeza uwezo kwa makundi ya wanawake na Asasi za kutetea haki za wanawake juu ya haki za wanawake, kimataifa, Africa na sheria za ndoa, mirathi na wosia Tanzania. Warsha hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Anglikana-Musoma tarehe 13-15 Agosti, 2013

Warsha hiyo iliendeshwa na na Asasi ya Women in Law and Development in Africa (WiLDAF). WiLDAF  ni mtandao, na Tanzania makao makuu yake yako Dar es Salaam, Mikocheni. Kila raia ana wajibu wa kufanya ili kulinda haki zake vinginevyo haki zake huweza kuvunjwa. Alisema mwezeshaji Destalia Haule kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). Bwana Aliko Sengo mwezeshaji toka WiLDAF aliseme elimu hii washiriki waliyoipata waipeleke katika jamii, na kutoa kisha wito



VIJANA KUKUTANA NA FURSA ZA MAENDELEO-MUSOMA





Pichani ni viongozi wa vikundi vya maendeleo ya vijana (vikundi 31) kutoka wilaya za Butiama na Musoma wakiwa na maafisa wa serikali na Asasi za kiraia katika picha ya pamoja ndani ya viwanja vya Kituo cha Matumaini katika Vijana-Manispaa ya Musoma


Maafisa hao ni pamoja na: Ndugu Adolfu Kami wa kwanza kushoto waliosimama mstari wa kwanza, afisa maendeleo ya vijana manispaa ya Musoma, ndugu Masatu Rugee, afisa michezo na utamaduni halimashauli ya wilaya ya Musoma, Afisa utawala na Fedha Ndugu Robert Moro, wa Shirika la Kutetea Haki za Wanawake na Watoto (ABC FOUNDATION); na Ndugu George Muyabi mratibu wa Mara Development Forum (MDF), pamoja na afisa mmoja wa CHODAWU na Idara ya Kazi na Ajira-Musoma
Asasi iliwakutanisha viongozi wa vikundi vya maendeleo ya vijana (vikundi 31) na maafisa hao kwa lengo la vijana hao kutambua fursa na wajibu wao ili waweze kunufaika na fursa zilizo katika ofsi za idara hizo za serikali 

“Kila kijana ni muhimu kutambua haki na wajibu wake; kila kijana ana haki na wajibu wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo yake bifsi, ya jamii pamoja na taifa kwa ujumla. Na kwa mantiki hii serikali, Asasi za kiraia, na jamii ni lazima kuhakikisha kuwa zinaweka mazingira rafiki (mazuri) kwa maendeleo yao na kushiriki kikamilifu katika Nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni”. Alisema Mkurugenzi wa Asasi ya Maendeleo ya vijana (TYPs-ASSOCIATION) Bwn. Japheth M. Kurwa
“Ili vijana waweze kunufaika na fursa za maendeleo ikiwemo mikopo itolewayo na serikali ni lazima wakizi vigezo stahili ambavyo ni pamoja na: usajiri angalau kwa ngazi ya Halmashauri, wawe na miradi na iwe halisi, miradi hiyo iwe rafiki wa mazingira, iwe na uwezo wa kupunguza umasiki, uelewa wa kikundi juu ya miradi hiyo, uwezekano wa mradi kulipa mkopo ndani ya miaka miwili, uwiano wa mkopo na mradi wenyewe, na upatikanaji wa soko la mazao ya miradi yao. Mikopo hii inalenga maendeleo ya vijana kwenye miradi hivyo ni muhimu kutambua kuna wajibu wa kufanya ili kunufaika na mikopo hiyo”. Alisema Ngudu Adolfu Kami, Afisa maendeleo ya vijana-Manispaa ya Musoma

“Kwa vijana wasio katika vikundi yya maendeleo, watengeneze vikundi ili kukizi vigezo vya kunufaika na fursa zinazokuja moja kwa moja kwenye vikundi na sio kwa mmoja mmoja. Na vikundi vyote vya maendeleo ya vijana viwe na njozi ya kujitengenezea fursa za ajira ili kupunguza umasikini uliokithiri. Vikundi ni lazima vijenge tabia ya uzalishaji na uwekezaji ili kuzalisha mitaji kwani vijana wengi ni wazuri kwa uzalishaji na matumizi hii haitawasaidia. Pia ni wakati sasa vikundi wa kuwa wanachama kwenye SACCOS ya Vijana na SACCOS nyingine ili viweze kupata mikopo ya mitaji kwa riba nafuu”. Alisema Ngugu Masatu Rugee, Afsa michezo na utamaduni Halimashauri ya wilaya ya Musoma.

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger