TANLAP YATOA MAFUNZO YA WATU WENYE ULEMAVU NA USULUHISHI MBADALA WA MIGOGORO
Saturday, March 29, 2014
Mtandao wa watoa msaada wa
kisheria (TANZANIA NETWORK OF LEGAL AID PROVIDERS-TANLAP) inaendesha mafunzo ya
sheria ya watu wenye ulemavu na usuluhishi mbadala wa migogoro, kwa wanachama
wake wapatao 60. Mafunzo yamefanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 27/3/2014
hadi 29/3/2014 katika Hotel ya Tamal jijini Dar es Salaam.
ü Siku
ya Kwanza: 27/3/2014: Sheria ya Watu wenye Ulemavu
ü Siku
ya Pili: 28/3/2014: Utatuzi wa Migogoro Kutumia Njia Mbadala
ü Siku
ya Tatu: 29/3/2014: Utatuzi Mbadala ya
Migogoro
Bwn. Gideoni Mandesi (Wakili),
kama mwezeshaji wa mafunzo sheria ya watu wenye ulemavu akifafanua Sheria Na. 9
ya mwaka 2010 alieleza makundi 7( Upofu, viungo, akili, kiziwi, ulemavu wa
ngozi, , uono hafifu na ulemavu wa viungo) ya walemavu na kusisitiza kwamba
pamoja na uwepo wa sheria hii Asasi za kiraia zina wajibu kisheria wa kufanya
ili sheria hii iwasaidie walengwa, na kusisitiza misingi ya sheria hii (Kifungu cha 4. (a)-(g) kama ifuatavyo.
a) Kuheshimu
utu, uhuru wa mtu
b) Kutobaguliwa
c) Kushurikishwa
katika nyaja zote katika jamii
d) Usawa
wa fursa
e) Ufikikaji
f) Usawa
wa kijinsia kwa kutambua haki na mahitaji ya walemavu
g) Kutoa
usalama na ulinzi wa kijamii
Adhabu kwa Unyanyapaa wa Walemavu
1) Kwa taasisi; faini isiyo chini ya shilingi
millioni mbili(2,000,000/=) na
isiyopungua shilingi million ishirini (20,000,000/=)
2) Kwa mtu binafsi; faini isiyopungua shilingi
laki tano (500,000/=) na isiyozidi shilingi milioni saba(7,000,000/=) au
Kufungwa jela
mwaka mmoja au vyote kwa pamoja
Bwn James Marenga (wakili),
mwezeshaji wa usuluhishi mbadala wa migogoro. Alitoa hatua 7 za ukuaji wa
migogoro
1) Kutokuwepo
taarifa na takwimu sahihi
2) Mahusiano
3) Thamani
4) Muundo
5) maslahi
Aidha alisisitiza ni vizuri na muhimu sana kila sahuli lipitie hatua ya usuluhishi mbadala wa migogoro kabla ya shauri hilo kwenda kwenye ngazi za mahakama na sheria inalitambua hilo na kulipa uzito. na kuwataka washiriki hao ambao ni wanachama wa mtandao huo kutumia njia mbadala wa usuluhishi wa migogoro kabla ya mashauri hayo kwenda mahakamani akibainisha na faida zake katika tathnia ya sheria.
HAKI YA KUISHI MATATANI KWA WANAWAKE MKOANI MARA
Sunday, February 2, 2014
Simanzi
na majozi vimeendelea kuikumba jamii ya mkoani Mara baada ya kuzuka Mauaji ya
kikatili ya kuchinja vichwa kwa wanawake, kunyongwa na hata kuondolewa sehemu
zao za siri ikiwa ni pamoja na kutobolewa macho kuendelea kushamili na kuifanya
Haki ya Kusishi kubaki kuwa kitendawili kwa wanawake mkoani Mara hususani
wilaya ya Butiama na Musoma. Mauji haya tangu kuzuka yapata ni mwaka mmoja sasa
(tangu 2013) na ufumbuzi wake ni sitofahamu.
Mama mmoja kwa jina Nyasatu Paulo
mwenye umri wa miaka 24, mkazi wa kijiji cha Kigera Etuma, Kata ya Nyakatende,
Tarafa ya Nyanja, Wilayani Butiama-Mara, alikutwa mauti shambani kwake kwa kifo
cha kunyongwa shingo na kisha kifukiwa kwa udongo wa matuta kama mzoga. Marehemu
alipotea siku moja kabla (tarehe 30/01/2014 Alihamisi) ya kupatikana mashambani
akiwa mauti (tarehe 31/01/2014 Ijumaa). Marehemu ameacha familia ya mume na
watoto 3, mdogo ( mtoto wa tatu) akiwa mwenye umri wa miezi 8.
Wanainchi
wenyeji wa maeneo ambamo mauaji haya hutokea wanabaini kuwa mauji haya
yanatokana na sababu kuu mbili:1. Imani za kishirikina, na ya 2. Visasi. Eidha
walibainisha kuwa Haki ya Usawa kwa wanawake pia imekuwa ndoana kwa wale
wanaodhubutu kuisimamia na kuidai hususani kumiliki au kurithi rasilimali mfano
ardhi, ng’ombe na nyumba.
Wanainchi
wameendelea kuitupia serikali lawama kuwa haijaamua kutokomeza mauaji haya ya
kikatili kwa wanawake yanayoendelea mkoani Mara. “Kama wanyamapori wanakufa na
Serikali inaanzisha Oparesheni Tokomeza kuzuia mauaji ya wanyamapori/Majangiri,
Je binadamu si rasilimali ya Taifa, mpaka ione haja ya kuwepo na Oparesheni ya
kutokomeza mauaji haya…?, Ni ajabu serikali yetu kuliacha swala hili kwa sehemu
kubwa mikononi mwa wanainchi!” Alisema Mkazi wa Kijiji cha Kigera Etuma kwa
Uchungu.
SECOND TANLAP ANNUAL GENERAL MEETING
The
meeting held on 28th January 2014 at LANDMARK Hotel, Dar es Salaam
from 08:00. Prior to the meeting there was a flections session to all TANLAP
members and other stakeholders to discuss on Access to Justice and Legal Aid in
Tanzania. The message of this meeting through t-shirts was “Tetea Wanyonge Dumisha Haki”
“Tanzania
Network of Legal Aid Providers (TANLAP) is an umbrella national network working
in legal sector. It is a network comprising of Non-Governmental Organizations
(NGOs), Community-Based Organizations (CBOs), Faith Based Organizations (FBOs)
and other institutions providing legal aid in Tanzania.
Founded
in 2006, TANLAP’s core aim is to work and link up with other Civil Society
Organizations provide quality legal aid and advocate for access to justice
among the poor and marginalized sections of society in Tanzania”. Said TANLAP
Secretary Ms. Christina Kamili
SIKU 16 ZA HARAKATI ZA KUPINGA UNYANYASAJI WA KIJINSIA DUNIANI (NOVEMBA 25- DESEMBA 10 KILA MWAKA)
Sunday, December 29, 2013
Siku 16 za harakati dhidi ya
ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa iliyoanzishwa na taasisi ya
kimataifa ya wanawake katika uongozi “ Womens Global Leadership Institute” ,
iliyoanzishwa mwaka 1991 nchini Marekani kwa nia ya kuamsha Ari ya kuzuiana
kupambana na ukatili dhidi ya wanawake, kwa kuzingatia haya ya kuleta usawa wa
kijinsia.
Kampeni hii ilianzishwa ikiwa ni
matokeo ya mauaji ya wanawake yaliyotokea 1960 Mirabele inchini Dominica,
wanawake hawa wakiwa katika harakati za kupinga utawala wa kidikteta wa Rais
wan chi hiyo Ndugu Raphaeli Truijilo, na kuhitimishwa tarehe 10 Desemba ambayo
ni siku ya kimataifa la tamko la haki za binadamu, ikiwa ni ishara ya kuhusisha
ukatili dhidi ya wanawake na haki za binadamu, kwani ukatili huu ni uvunjivu wa
haki za binadamu
Kati ya tarehe 25/11/ hadi Tarehe
10/12 ya kila mwaka, kuna matukio mbalimbali ya kimataifa, ambayo ni sehemu
muhimu katika kuleta ukombozi kwa jamii, hasa wanawake juu ya ukatili wa
kijinsia. Baada ya matukio hayo, ni pamoja na siku ya kimataifa ya wanawake
watetezi wa haki za binadamu 29/11 ya kila mwaka, Desemba 1 siku ya UKIMWI
duniani, Desemba 6 kumbukumbu ya mauaji ya kikatili ya wanawake wahandisi mjini
Montreal nchini Canada, tarehe 30 Desemba siku ya kidunia ya Kampeni ya
Tunaweza, inayolenga kuondoa ukatili wa aina zote dhidi ya wanawake na Desemba
10 siku ya tamko la haki za binadamu kimataifa
Kwa sababu hizi siku 16 za
harakati za kupinga unyanyasaji wa kijinsia duniani huazimishwa Novemba 25-
Desemba 10 kila mwaka.
TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFENDERS’S DAY
TANZANIA HUMAN RIGHTS
DEFENDERS’S DAY
TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFFENDERS
COALITION has launched THE TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFFENDERS’S DAY on 12th
December, 2013 At Double View Hotel in Dar es Salaam City. 12th
December each year shall be the day of human rights defender’s Day.
Mr. Onesmo Paul Olengulumwa the
National Coordinator of THRD-Coalition gave the Concept of Human Rights
Defenders Day and then issued awards to selected HRDs ending with the message
of “A Human Right Defender is Better Alive than Dead”
Dr Helen Kij-Bisimba-LHRC, said
Human Rights Defenders should be confident; boldness, courage and fearless.
Assurance and confidence do not anchor us in our selves but in what we do. Key
note addressed by the Specially Guest- Justice Amir Manento CHRAGG Chairperson