SIKU 16 ZA HARAKATI ZA KUPINGA UNYANYASAJI WA KIJINSIA DUNIANI (NOVEMBA 25- DESEMBA 10 KILA MWAKA)

Sunday, December 29, 2013



Siku 16 za harakati dhidi ya ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa iliyoanzishwa na taasisi ya kimataifa ya wanawake katika uongozi “ Womens Global Leadership Institute” , iliyoanzishwa mwaka 1991 nchini Marekani kwa nia ya kuamsha Ari ya kuzuiana kupambana na ukatili dhidi ya wanawake, kwa kuzingatia haya ya kuleta usawa wa kijinsia.
Kampeni hii ilianzishwa ikiwa ni matokeo ya mauaji ya wanawake yaliyotokea 1960 Mirabele inchini Dominica, wanawake hawa wakiwa katika harakati za kupinga utawala wa kidikteta wa Rais wan chi hiyo Ndugu Raphaeli Truijilo, na kuhitimishwa tarehe 10 Desemba ambayo ni siku ya kimataifa la tamko la haki za binadamu, ikiwa ni ishara ya kuhusisha ukatili dhidi ya wanawake na haki za binadamu, kwani ukatili huu ni uvunjivu wa haki za binadamu
Kati ya tarehe 25/11/ hadi Tarehe 10/12 ya kila mwaka, kuna matukio mbalimbali ya kimataifa, ambayo ni sehemu muhimu katika kuleta ukombozi kwa jamii, hasa wanawake juu ya ukatili wa kijinsia. Baada ya matukio hayo, ni pamoja na siku ya kimataifa ya wanawake watetezi wa haki za binadamu 29/11 ya kila mwaka, Desemba 1 siku ya UKIMWI duniani, Desemba 6 kumbukumbu ya mauaji ya kikatili ya wanawake wahandisi mjini Montreal nchini Canada, tarehe 30 Desemba siku ya kidunia ya Kampeni ya Tunaweza, inayolenga kuondoa ukatili wa aina zote dhidi ya wanawake na Desemba 10 siku ya tamko la haki za binadamu kimataifa
Kwa sababu hizi siku 16 za harakati za kupinga unyanyasaji wa kijinsia duniani huazimishwa Novemba 25- Desemba 10 kila mwaka.


Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger