VIJANA MANISPAA YA MUSOMA KUAZIMIA KUUNDA CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPO

Monday, April 14, 2014





CHAMA CHA USHIRIKA CHA AKIBA NA MIKOPO CHA VIJANA MUSOMA SACCOS (VIMU SACCOS) LTD
S.L.P …., Musoma-Mara. Simu: 0756290672, 0755671818, & 0654655498

Vijana wapatao 45, manispaa ya Musoma wameazimia kuunda na kusajiri Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo kijulikanacho kwa jina la VIJANA MUSOMA SACCOS LTD kwa lengo la kuinuana khali zao kiuchumi na kijamii.
Mwenyekiti wa Bodi ya uanzilishi wa Chama hicho, Bwn. Japheth M. Kurwa; alisema “Wanachama wa chama cha ushirika cha VIJANA MUSOMA SACCOS (VIMU SACCOS) tumeamua rasmi na kwa dhati kusaidiana, kushirikiana, kuthaminiana, kujaliana, kujiendeleza na kusimamia ubora wa maisha yetu ili kila mmoja apate unafuu na furaha katika maisha kwa kuzingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani, Madhumuni ya chama hiki cha ushirika ni kuinua na kuimarisha hali ya kiuchumi na kijamii ya wanachama wake (Vijana) kwa kufuata kanuni na taratibu za vyama vya ushirika. Hivyo basi napenda kutoa wito kwa vijana wote wa manispaa ya Musoma kujiunga na Chama hiki. Vijana Musoma SACCOS ni kwa Ajiri ya Maendeleo yako Binafsi, Familia yako, Jamii yako, na Taifa kwa Ujumla.
“Weka Akiba Mara kwa Mara, Kopa kwa Busara, Lipa Upesi”

Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger