KILIMO KAMA MKOMBOZI WA VIJANA NI CHANGAMOTO

Thursday, September 19, 2013

Kijana Esogo Kubega, mkazi wa Kigera-Manispaa ya Musoma, akijibidisha katika shughuli za kilimo cha bustani kama ajira yake. Japo mafanikio yapo lakini nina changamoto kubwa ya maji kwani maji haya ni ya dibwini na upatikana kwa muda mfupi tu mara baada ya musimu wa mvua, Mungu akinifungulia milango nikapata kuchimba kisima cha kudumu na mashine ya kumwagilia naamini sitokuwa na haja ya kuajiliwa kwani hapa ndipo penye riziki yangu. Lakini pia nina changamoto ya magonjwa, mwaka jana nililima tikiti maji zikashambuliwa na wadudu na mwaka huuu nimebadilisha na kulima nyanya nako tazama zilivyoshambuliwa na wadudu, hii yote ni ukosefu wa mitaji. Mbona mkoa wa Mara sera ya kilimo kwanza siioni au ni maalumu kwa mikoa Fulani tu, kama ni ya kitaifa basi itukumbuke nasi pia twahiitaji, Alisema Kijana Esogo Kubega.
Napenda kumshukuru Bw. Kurwa, mkurugenzi wa Asasi ya Maendeleo ya Vijana na Haki za Wanawake na Watoto (TYPs-ASSOCIATION) kwa kutuwezesha kupata elimu ya ujasilia mali kwa kiasi kikubwa elimu hii imetupa mwanga mkubwa wa kazi zetu za kilimo na ujasilia mali. Wakipatikana watu kama hawa 10 mbona ukombozi kwa vijana umepatikana. Ugumu ni kujitafutia mtaji mwenyewe na khali huna hata mia mfukoni kwangu mimi mtaji ni kikwazo kikubwa sana ningekuwa mbali, Esogo alizidi kusema. Picha na TYPs-ASSOCIATION



Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger