SIKU 16 ZA HARAKATI ZA KUPINGA UNYANYASAJI WA KIJINSIA DUNIANI (NOVEMBA 25- DESEMBA 10 KILA MWAKA)
Sunday, December 29, 2013
Siku 16 za harakati dhidi ya
ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa iliyoanzishwa na taasisi ya
kimataifa ya wanawake katika uongozi “ Womens Global Leadership Institute” ,
iliyoanzishwa mwaka 1991 nchini Marekani kwa nia ya kuamsha Ari ya kuzuiana
kupambana na ukatili dhidi ya wanawake, kwa kuzingatia haya ya kuleta usawa wa
kijinsia.
Kampeni hii ilianzishwa ikiwa ni
matokeo ya mauaji ya wanawake yaliyotokea 1960 Mirabele inchini Dominica,
wanawake hawa wakiwa katika harakati za kupinga utawala wa kidikteta wa Rais
wan chi hiyo Ndugu Raphaeli Truijilo, na kuhitimishwa tarehe 10 Desemba ambayo
ni siku ya kimataifa la tamko la haki za binadamu, ikiwa ni ishara ya kuhusisha
ukatili dhidi ya wanawake na haki za binadamu, kwani ukatili huu ni uvunjivu wa
haki za binadamu
Kati ya tarehe 25/11/ hadi Tarehe
10/12 ya kila mwaka, kuna matukio mbalimbali ya kimataifa, ambayo ni sehemu
muhimu katika kuleta ukombozi kwa jamii, hasa wanawake juu ya ukatili wa
kijinsia. Baada ya matukio hayo, ni pamoja na siku ya kimataifa ya wanawake
watetezi wa haki za binadamu 29/11 ya kila mwaka, Desemba 1 siku ya UKIMWI
duniani, Desemba 6 kumbukumbu ya mauaji ya kikatili ya wanawake wahandisi mjini
Montreal nchini Canada, tarehe 30 Desemba siku ya kidunia ya Kampeni ya
Tunaweza, inayolenga kuondoa ukatili wa aina zote dhidi ya wanawake na Desemba
10 siku ya tamko la haki za binadamu kimataifa
Kwa sababu hizi siku 16 za
harakati za kupinga unyanyasaji wa kijinsia duniani huazimishwa Novemba 25-
Desemba 10 kila mwaka.
TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFENDERS’S DAY
TANZANIA HUMAN RIGHTS
DEFENDERS’S DAY
TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFFENDERS
COALITION has launched THE TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFFENDERS’S DAY on 12th
December, 2013 At Double View Hotel in Dar es Salaam City. 12th
December each year shall be the day of human rights defender’s Day.
Mr. Onesmo Paul Olengulumwa the
National Coordinator of THRD-Coalition gave the Concept of Human Rights
Defenders Day and then issued awards to selected HRDs ending with the message
of “A Human Right Defender is Better Alive than Dead”
Dr Helen Kij-Bisimba-LHRC, said
Human Rights Defenders should be confident; boldness, courage and fearless.
Assurance and confidence do not anchor us in our selves but in what we do. Key
note addressed by the Specially Guest- Justice Amir Manento CHRAGG Chairperson
VIJANA MUSOMA SACCOS (VIMUSA)
Tuesday, November 19, 2013
Wanachama wa
chama cha ushirika cha VIJANA MUSOMA
SACCOS (VIMUSA) tumeamua rasmi na kwa dhati kusaidiana, kushirikiana,
kuthaminiana, kujaliana, kujiendeleza na kusimamia ubora wa maisha yetu ili
kila mmoja apate unafuu na furaha katika maisha kwa kuzingatia misingi ya
uhuru, haki, undugu na amani.
ENEO LA SHUGHULI
Eneo la
shughuli za chama ni wilaya ya Musoma mjini, lakini hata wanachama walioko nje ya eneo la wilaya
watashiriki kama wataweza kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama
MADHUMUNI
Madhumuni ya
chama hiki cha ushirika ni kuinua na kuimarisha hali ya kiuchumi na kijamii ya
wanachama wake kwa kufuata kanuni na taratibu za vyama vya ushirika. Ili
kufanikisha madhumuni haya, ushirika huu
wa Akiba na Mikopo utafanya yafuatayo:-
a)
Kuhamasisha wanachama wake kujenga tabia ya kujiwekea akiba
mara kwa mara
b)
Kupokea na kutunza akiba na amana za wanachama kwa njia
rahisi na salama
c)
Kutafuta vyanzo vya fedha ili kujenga na kuimarisha
mtaji kwa ajili ya kutoa mikopo kwa
wanachama kwa masharti na riba nafuu
d)
Kuwaelimisha wanachama kujijengea tabia ya kukopa kwa busara
na kutumia vizuri mikopo na kuinua hali zao za maisha kiuchumi na kijamiii.
e)
Kutoa bidhaa mbalimbali za fedha(financial products) kwa
wanachama ili waweze kushiriki zaidi kuimarisha mitaji ya chama na mitaji yao
binafsi ili waweze kuleta mvuto kwa wasio wanachama kujiunga na chama
f)
Kuweka kwa usalama fedha za chama na za wanachama kwa
kuanzisha mipango kwa kukabiliana na
majangana/au kuweka bima za fedha zinazofaa
g)
Kuwashauri wanachama
kuandaa mipango yao ya maendeleo katika kuwekeza mitaji kwenye miradi ya
kiuchumi na huduma za jamii
h)
Kutoa elimu ya ushirika kwa wanachama
i)
Kufanya mambo mengine ambayo yataendeleza hali ya uchumi wa
chama na wanachama
j)
Kuwaelimisha wanachama umuhimu wa kutumia fedha zao kwa
mipango, kuweka hakiba, kukopa kwa ajiri maendeleo ya biashara na kilimo kupiga
vita tabia ya ufujaji mali na matumizi mabaya ya fedha
UANACHAMA
Mtu yeyote
anaweza kuwa mwanachama akiwa na sifa zifuatazo:-
a)
Awe na umri usiopungua miaka 18. Mtu yeyote mwenye umri
usiopungua miaka 15 anaweza kuwa mwanachama isipokuwa hataruhusiwa kukgombea
uongozi na kukopa mpaka atakapotimiza miaka 18
b)
Awe na akili timamu
na tabia njema
c)
Awe anafanya kazi au shughuli yoyote halali na awe mkazi wa
eneo la chama na kufuata masharti ya chama
d)
Awe tayari kushiriki kikamilifu katika shughuli zote za
chama
e)
Asiwe na shughuli binafsi zinazofanana na shughuli za chama
f)
Kikundi/Chama/Taasisi/Asasi yenye sifa za kujiunga na chama
hiki kwa mujibu wa sheria ya vyama vya ushirika,kanuni za vyama vya ushirika
pamoja na masharti haya
g)
Awe mfanyakazi au mtumishi wa chama
h)
Awe amelipa kiiingilio
(5,000/-)na kununua kima cha chini cha hisa
(Hisa 1@ 10,000/-)
CHANGAMOTO
Kuna
changamoto kubwa kwa vijana kama wanufaika:-
Ø
Vijana wengi
hawapo katika ngazi za maamuzi, matokeo yake maamuzi mengi hayagusi matakwa ya
vijana
Ø
Vijana wengi
hawana utayari ulio thabiti na wa kweli, wa kushiriki kuibua fursa na kuzitumia
ipasavyo
Ø
Vijana wengi hasa
miji midogo hawana tabia ya “kuwekeza na kuzalisha”, wengi wanadesturi ya
kutumia kidogo walichonacho kwa kauli kama vile: tumia pesa ikuzoee, elfu moja
haijengi n.k
Bado
hatujachoka,ni kwamba vijana hawana elimu ya ujamaa(umoja na udugu) na
kujitegemea tutazidi kuwahamasisha vijana kutumia fursa ya SACCOS ya vijana manispaa ya Musoma kwa maana
ya VIJANA MUSOMA SACCOS (VIMUSA) kujiunga
na SACCOS hii yenye nia ya kukuza mitaji kwa vijana ili waweze kujiajiri.
“Weka
Akiba Mara kwa Mara, Kopa kwa Busara, Lipa Upesi”
Japheth
M. Kurwa
Mob: 0756290672 & 0712547199 Email: kurwajapheth@gmail.com
Mwenyekiti, VIMUSA
Mob: 0756290672 & 0712547199 Email: kurwajapheth@gmail.com
Mwenyekiti, VIMUSA
MIDAHALO YA WAZI NA SINEMA KUZUIA UKATILI WA KIJINSIA
Thursday, September 26, 2013
TYPs-ASSOCIATION (Asasi ya Maendeleo ya Vijana na Haki za Wanawake na Watoto) wakishirikiana na SHirika ya ABC
Foundation(Shirika la Kutetea Haki za Wanawake na Watoto) chini ya kampeni ya TUNAWEZA. Kampeni hii iliweza Asasi na wadau mbalimbali kuvunja ukimya juu ya ukatili majumbani na jamii kuona kwamba ukatili si sehemu ya maisha, hata hivyo jamii ilitambua maana, aina na nini kifanyike kutokomeza ukatili wa kijinsia/nyumbani.
Kampeni ya TUNAWEZA Tanzania
inasimamiwa na Oxfam, WLAC, KIVULINI na Haki Madini ikitekelezwa na wadau
mbalimbali wa mashirika haya, ikiwa ni pamoja na ABC Foundation (Shirika la
Kutetea Haki za Wanawake na Watoto) chini ya Shirika la KIVULINI. Lengo Kuu la
Kampeni ya Tunaweza: Kupunguza Ile Khali ya
Jamii Kuona Ukatili ni Kitendo cha Kawaida au ni Sehemu ya Maisha. Jamii
itambue kuwa kwa pamoja tunaweza kuondoa aina zote za ukatili wa
kijinsia/nyumbani.