Karibu Musoma Information Center kwa huduma zifuatazo:- 1) Kwa kutengenezewa design mbalimbali kama za Business card, Vipeperushi, mabango mbalimbali, kadi za Harusi za kisasa zaidi, kadi za mialiko mbalimbali, Vitambulisho vya wanafunzi wa sekondari na katika kampuni mbalimbali ( ID cards) na kadi nyinginezo zenye design ya kuvutia. 2) Kutengenezewa mabango ( Posters) mbalimbali zinazohusu biashara ya mhusika au bidhaa mbalimbali. 3) Kutengenezewa nembo ( LOGO) za kuhusiana kampuni au biashara yako. 4) Tunatengeneza tovuti ( Websites ) zenye kiwango ambacho huwezi amini kama zinatengenezwa musoma, kwa bei nafuu ambayo huwezi ipata kwingine isipo kuwa kwetu. 5) Mwisho tunatoa ushauri na elimu kuhusiana na maswala ya computer.5) Sisi ni watengenezaji wa blog zinazokaa mfumo wa website. kama hii unayoiona.

Welcome to TYPS - ASSOCIATION

Welcome to TYPS - ASSOCIATION

Welcome

A Letter from the Executive Director

Dear All,

As Executive Director it is my pressure to welcome you to TANZANIA YOUTH POTENTIALS ASSOCIATION (TYPs-ASSOCIATION)-a growing youth-led Organization with it’s headquarter in Musoma that operates through legal registration number 00NGO/00006304 under the ACT of 2002 in Tanzania. The focus of the organization is to utilize youth’s potentials for their own development, community and state development at large. It also intends to strengthen regional and international interventions towards protection and promotion of the human rights especially to children, youth and women. It works with networking with other partners/ stakeholders and beneficiaries.

The Organization has the mission of striving and inheriting youth and other community groups with various technical capacities eligible to make them be engines for socio-economic growth for individual benefits, societies and the national at large as such to see a community in which women’s and children’s rights are observed and respected by executing mobilization projects eligible to bring positive changes to community through action and participation in collaboration with community and other stakeholders to prevent Gender Based Violence (GBV).

However the organization is dedicated to develop dynamic and entrepreneurial youths who will engage and realize their full potential and that of their community, their country and the world at large and advocating The National Youth Development Policy

The Secretariat , the Board of Directors and the Annual General Meeting of TYPs-ASSOCIATION eagerly anticipate your arrival and contribution to its future, and welcome you to discover youth development experience that promotes your Personal and intellectual growth

Welcome to TYPs-ASSOCIATION,
Mr. Japheth M. Kurwa
Executive Director


Saturday, July 1, 2017

Ivi ni vikundi vya ujasiriamamli kata ya chamanzi manispaa ya Temeke wakijifunza utengenezaji wa sabuni za maji, mafunzo haya yalitolewa na wakufunzi willson mwilinge na Dismass nyamanda
Mafunzo haya yalifanyika katika ukumbi wa COMFORT uliopo chamanzi Tarehe 27-28 mwezi june 2017.

TANZANIA YOUTH POTENTIAL ASSOCIATION  wakitoa mafunzo ya ujasiliamali katika kata ya Chamanzi manispaa ya Temeke wakishirikiana na Maendeleo Bank. Mafunzo hayo yalifanyika tarehe 27-28 mwezi Juni 2017,Mafunzo hayo ya ujasiliamali yalikuwa na washiriki 65

Tuesday, May 23, 2017

Friday, March 31, 2017

MAFUNZO YA UJASILIAMALI YANAYOTOLEWA NA TANZANIA YOUTH POTENTIALS ASSOCIATION

HAYA NI MAFUNZO YALIYOTOLEWA MKOA WA PWANI WILAYA YA MKULANGA
 HAWA NI WAJASILIAMALI WA WILAYA YA MKULANGA WAKIPATA MAFUNZO YA UJASILIAMALI
LENGO LA MAFUNZO HAYA NI KUISAIDIA JAMII IWEZE KUJIKOMBOA KIUCHUMI
MAFUNZO HAYA YALIFANYIKA TAREHE 29/12/2016 KATIKA WILAYA YA MKULANGA
 HAYA NI MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WA KUJIAJIRI VIJANA YALIYOTOLEWA MKOA WA DAR ES SALAAM, MANISPAA YA ILALA, KATA YA 
GONGO LA MBOTO.
 MAFUNZO HAYA YA UJASILIAMALI YALIFANYIKA TAREHE 3/11/2016
VIJANA MNATAKIWA MTUMIE FURSA HII MUWEZE KUNUFAIKA

 HIZI NI BIDHAA AMBAZO TUNAWAFUNDISHA WAJASILIAMALI UTENGENEZAJI WA SABUNI,UTENGENEZAJI WA SWETA,NA N.K.  TAASISI YETU INA WAKUFUNZI BORA AMBAO WANATOA MAFUNZO YENYE VIWANGO VIZURI
TAASISI YETU INATOA MAFUNZO YA KILIMO KWA WAJASILIAMALI  
 TANZANIA YOUTH POTENTIALS ASSOCIATION INAPATIKANA MUSOMA AMBAPO NI MAKAO MAKUU NA TAWI LAKE LIPO DAR ES SALAAM, MANISPAA YA ILALA KATA YA GONGO LA MBOTO KARIBUNI VIJANA NA AKINA MAMA MPATE MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WA KUJIAJIRI 
MAWASILIANO:
0714-845940/0758 679661
TAASISI YETU IMEKUWA IKITOA MSAADA KWA VIKUNDI MBALIMBALI IKIWEMO VITENDEA KAZI VYA UJASILIAMALI KAMA VILE MALI GHAFI ZA UTENGENEZAJI WA SABUNI, ZANA ZA KILIMO, MIKOA ILIYONUFAIKA NI MKOA WA PWANI, WILAYA YA MKULANGA ,MKOA WA MARA WILAYA YA TARIME NA SERENGETI. HIZI NI WILAYA AMBAZO ZIMENUFAIKA NA MIRADI YETU 

 HAYA NI MAFUNZO YA UJASILIAMALI YALIYOFANYIKA KATIKA MKOA WA MARA WILAYA YA MUSOMA VIJIJINI YALIFANYIKA MWEZI WA 8 MWAKA 2016 LENGO LILIKUWA KUISAIDIA JAMII IONDOKANE NA UMASIKINI
TUNATOA MAFUNZO YA UTENGENEZAJI WA MIZINGA YA UDONGO AMBAYO NI BORA KWA UFUGAJI WA NYUKI 
 TANZANIA YOUTH POTENTIALS ASSOCIATION TUMEKUWA TUKISHIRIKIANA NA TAASISI MBALIMBALI KUFANYA KAZI ZA KIJAMII KAMA VILE JUHUDI FOUNDATION,MWAMBAO ORGANIZATION, INTERNATIONAL EDUCATORS TRUST FUND TANZANIA,NA TUWAFIKIE TANZANIA. TUNAZIKARIBISHA TAASISI MBALIMBALI TUWEZE KUFANYA KAZI ZA KIJAMII  
UANDAAJI WA BWAWA LA SAMAKI
BWAWA LA SAMAKI AMBALO LIMESHAKAMILIKA
 HAYA NI MABWAWA AMBAYO YAMEKOSA MAJI TUNAWAKARIBISHA WAJASILIAMALI MUWEZE KUJIFUNZA UFUGAJI WA SAMAKI NA ATHARI ZAKE

TYP INATOA NAFASI ZA KUJITOLEA LENGO NI KUWAJENGEA UWEZO VIJANA WA KUFANYA KAZI ZA KIJAMII NA KUWA NA UWEZO MBALIMBALI WA TAALUMA ZAO
MWISHO WA MAOMBI HAYA NI TAREHE 6/5/2017 KWA MAWASILIANO
0714 845940/0758 679661






16 Days of Activism 2016

Sunday, November 6, 2016



UN Women – United Nations Entity for Gender Equality and the Empowerment of Women

16 days of activism   2016

From 25 November, the International Day for the Elimination of Violence against Women, to 10 December, Human Rights Day, the 16 Days of Activism against Gender-Based Violence Campaign is a time to galvanize action to end violence against women and girls around the world. The international campaign originated from the first Women's Global Leadership Institute coordinated by the Center for Women's Global Leadership in 1991.
In 2016, the UNiTE campaign strongly emphasizes the need for sustainable financing for efforts to end violence against women and girls towards the fulfilment of the 2030 Agenda for Sustainable Development.
One of the major challenges to efforts to prevent and end violence against women and girls worldwide is the substantial funding shortfall. As a result, resources for initiatives to prevent and end violence against women and girls are severely lacking. Frameworks such as the Sustainable Development Goals, which includes a specific target on ending violence against women and girls, offer huge promise, but must be adequately funded in order to bring real and significant changes in the lives of women and girls.
To bring this issue to the fore, the UN Secretary-General’s campaign UNiTE to End Violence against Women’s call for the 16 Days of Activism against Gender-Based Violence in 2016 is ‘Orange the World: Raise Money to End Violence against Women and Girls’. The initiative provides a moment to bring the issue of sustainable financing for initiatives to prevent and end violence against women to global prominence and also presents the opportunity for resource mobilization for the issue.
The United Nations Official Commemoration of the International Day for the Elimination of Violence against Women will take place on 21 November from 10 a.m. – 12 p.m. EST. Save the Date!


“Copied from UN WOMEN “

PROGRAM YA UHAMASSHAJI NA MAFUNZO KWA VIJANA.

Friday, January 9, 2015



PROGRAM YA UHAMASSHAJI NA MAFUNZO KWA VIJANA.
Katika mikakati ya kuhamasisha vijana na kuwawezesha kiuchumi, na kijamii, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imeandaa na kuendesha program ya mafunzo kwa vijana.  Tar 22-24, Desemba 2014 maafisa wa wizara walikuwa mkoani Arusha wakitoa mafunzo hayo kwa halimashauri ya Arusha Jiji, Arusha DC, Meru na Monduli.
Kutokana na umuhimu wa mafunzo haya halimashauri zilizobaki zinatakiwa kuendesha mafunzo haya ifikapo Februari 30, 2015, kwa kushirikiana na maafisa wa mkoa na halmashauri husika. Mada zilizofundishwa ni pamoja na:-
             i.        Sera ya taifa ya maendeleo ya Vijana ya mwaka 2007
            ii.        Stadi za maisha
           iii.        Dhima ya uanzishwaji wa SACCOS za vijana
           iv.        Mwongozo wa uandaaji katiba
            v.        Mwongozo wa utoaji wa mikopo ya mfuko wa maendeleo ya vijana kwenye miradi
           vi.        Usajiri wa vikundi vya vijana
         vii.        Namna ya kuandika miradi
Mada zote nimeziambatanishwa jiandaeni kufanikisha zoezi hili. Aidha mambo ya msingi yatokanayo ni:-
     i.        Mikopo ya vijana toka mfuko wa vijana unaosimamiwa na wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Kwa kuanzia wizara imetenga kiasi cha shilingi milioni 30 kwa vikundi 3 kila halmashauri na fedha hizo zitapita kwenye SACCOS za vijana.
    ii.        Uanzishwaji wa SACCOS ya vijana kwa kila halimashauri. Mpaka sasa ni halimashauri tatu tu zilizotekeleza agizo hili kati ya halmashauri saba; ambazo ni halmashauri ya Karatu; SIMBA MASAI SACCOS LTD, Halmashauri ya Meru; MERU VIJANA SACCOS LTD; na Halmashauri ya Longido; LONGIDO VIJANA SACCOS LTD.
Halmashauri zilizokwisha sajiri SACCOS za vijana ifikapo tarehe 30 Januari, 2015 ziwe zimekwisha wasilisha maandiko ya miradi yasiopungua manne kwa Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa tayari kutumwa wizarani.
Sambamba na haya utekelezaji wa agizo la Rais katika sherehe za maadhimisho ya kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru 2014 mkoani Tabora kuhusu maswala ya vijana ikiwa ni pamoja na zoezi la uanzishwaji wa SACCOS za Vijana kama ifuatavyo:-
             i.        Kutenga 5% ya mapato ya halmashauri kwa ajili ya kuwawezesha vijana. Naomba utekelezaji wake ipasavyo.
            ii.        Maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli za vijana ili kujikwamua kiuchumi; hususani shughuli za kilimo na biashara.

"VIJANA TUNAO WAJIBU WA KUFANYA"

UZINDUZI: SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA 2014

Friday, November 21, 2014



Umma wa watanzania wanaharakati wa kupinga vitendo vya Ukatili wa Kijinsia jumanne tarehe 25, Novemba 2014 watazindua kampeni hii kitaifa, kimkoa na maeneo mbalilmbali ya kiutendaji.  Hii ni kampeni ya siku 10 na huzinduliwa tarehe 25, Novemba ya kila mwaka hadi tarehe 10, Desemba.

Kitaifa itazinduliwa pale Viwanja vya Karimjee kuanzia saa 3 asubuhi. Uzinduzi huu utafuatana  na maandamano ya amani yakihamasisha jamii kuachana na Vitendo vya Ukatili wa Kijinsia, kuanzia viwanja vya mnazi mmoja kupitia, barabara ya Morogoro, barabara ya Bibi Titi Mohamed, Ali Hassan Mwinyi,Mtaa wa Ohio, Samora hadi Viwanja vya Karimjee. Yote haya yataanza saa 1:30 asubuhi.

Kauli Mbiu ya mwaka huu ni “FUNGUKA! FICHUA UKATILI WA KIJINSIA KWA AFYA YA JAMII” ,Katika Kiingereza, “OPEN UP! DISCLOSE GENDER BASED VIOLENCE FOR THE HEALTH OF THE COMMINITY”

Kampeni hii kitaifa inaratibiwa na Shirika na WiLDAF kwa kushirikiana na Wadau toka Irish AID na UN Women.

Watanzania tupinge Vitendo vyote vya Ukatili wa Kijinsia, vitendo hivi huongeza mzigo kwa maendeleo ya jinsi zote, familia, jamii husika na taifa kwa ujumla.

AJIRA: VIJANA AMBAO HAWAKUBAHATIKA KUENDELEA NA MASOMO.




Kundi hili ni kundi linalojumuisha vijana wengi zaidi kuliko lile la vijana wasomi. Vijana wengi walioko katika kundi hili ni wale walioko katika ajira zisizo lasmi kama vile; uvuvi, kilimo, kubeba mizigo, ufugaji, machinga, garage, udereva wa magari na pikipiki (Bodaboda), ulinzi, vibarua vya ujenzi, vibarua katika sekta ya madini, migahawa/ vibanda vya lishe na kuchoma chips, saloon, uselemala, vibarua viwandani n.k
1.   Tafsiri Baadhi ya Maneno
Ajira: Ni shughuli yoyote halali (rasmi au isiyo rasmi), inayomwezesha mwananchi kujipatia riziki, mahitaji na kipato cha kuendesha maisha yake, ya familia na pengine kuchangia katika pato la eneo alipo au Taifa.
Kutokuwa na ajira: Ni hali ya kukosa kazi kabisa au nguvukazi iliyopo kutotumika kuzalisha mali au kutoa huduma.
 Kijana: Zipo tafsiri aina mbili;
i)    Kimataifa; Kijana ni mtu mwenye umri wa miaka 15 hadi 24
ii)   Kwa Tanzania ni miaka 15 hadi 35
Sekta isiyo rasmi: Hii ni sekta ambayo si ya shambani wala ofisini, ya kiwango cha chini na ya kujiajiri   inayotumia mtaji na teknolojia ndogo.
Fursa: Ni shughuli za kiuchumi na kijamii au za uzalishaji mali au huduma ambazo hutekelezwa na mtu na kuweza kumpatia kipato halali.

2.   Fursa ya Uvuvi na Uzaji wa Samaki-Kisiwani Lukuba
Sekta ya Uvuvi ni moja ya sekta iliyoajiri vijana wengi hapa Tanzania, Kisiwa cha lukuba ni moja ya Visiwa vilivyoko mkoani Mara chenye fursa kubwa ya ajira ya kujiajiri.
Kisiwa hiki kinatoa fursa nyingi za ajira ya kujiajiri kwa vijana hususani wale ambao hawakubahatika kwendelea na masomo. Fursa za ajira ni uvuvi unaoambatana na usafirishaji, uchakataji, uchuuzi wa samaki na uzalishaji viwandani, ujenzi wa mitumbwi/boti za uvuvi.
Kisiwa hiki kinategemea shughuli ya uvuvi na uuzaji wa samaki hususani samaki aina ya Dagaa na Sangara (Nile perch). Uvuvi katika kisiwa hiki unatoa mchango mkubwa katika kuinua kiwango cha maisha ya vijana hawa, wananchi wa Musoma na nchi kwa ujumla. Hata hivyo, fursa bado ni kubwa kwa wawekezaji wengi kuwekeza katika eneo hili.
Serikali inatakiwa kuongeza juhudi za makusudi kuhakikisha uendelevu wa raslimali ya uvuvi ambayo ni msaada mkubwa kwa taifa. Aidha inatakiwa kuliangalia eneo hili kwa makini ili kuwawezesha vijana hususani kundi hili ambalo halikubahatika kuendelea na masomo yao.

3.   Changamoto ya Jumla Kuhusu Ajira ya Vijana ambao Hawakubahatika Kuendelea na Masomo.
Kundi hili ni kundi linalojumuisha vijana wengi zaidi kuliko lile la vijana wasomi, kwa mtazamo wa haraka kundi hili la vijana ni kama limesahulika.; changamoto zinazolikabili kundi hili ni pamoja na:-
·         Hali ya kutokuwa na fursa ya kushiriki katika uchumi inayosababishwa na uwezo mdogo katika mitaji, ukosefu wa ujuzi na uzoefu wa biashara, pamoja na matatizo yanayohusiana na kutokopesheka.
·         Hali ya kutopata fursa ya kushiriki katika fursa za kiuchumi katika mfumo rasmi
·         Kutopokelewa na jamii katika mtazamo chanya; kunakoleta tafasili kandamizi kwao kama vile tafasiri ya wahuni na watu waliofeli maisha, tafasili ambayo hupelekea vijana hao kuwa hivyo.
·         Uhusiano mdogo wa kundi hili na sekta rasmi, taasisi binafsi na za umma; na Serikali kwa ujumla

4.   Nini Kifanyike
Wadau wote wa maendeleo ya vijana (serikali, jamii, sekta binafsi, Asasi za kijamii, familia na vijana wenyewe) kuwa karibu sana na kundi hili kama walezi na walimu; na kutekeleza wajibu huu ipasavyo

Vijana kuchangamkia fursa na kuzitumia ipasavyo katika kuwekeza na kuzalisha (Saving and Production). Ogopeni semi kama vile: Tumia pesa ikuzoee, elfu moja haijengi, raha jipe mwenyewe, kula ujana maisha yenyewe mafupi n.k

Maeneo haya yenye kuwaajiri vijana walioko katika kundi hili, yakipewa kipaumbile na kutengenezwa kuwa mazingira rafiki ya kujiajiri yatapunguza kwa kiasi kikubwa kero ya ajira kwa vijana na taifa kwa ujumla.

By: Mr. Japheth M. Kurwa
Falsafa yangu ni:- “JUHUDI ZISIZOKOMA KATIKA KUJIFUNZA NA KUFANYA KAZI”

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger