Chanzo cha habari Udakuespecially
CLOUDS FM YAKANUSHA KUHUSU MWANA FA KUAHIRISHA SHOW YAKE YA THE FINEST LEO HII
Friday, June 14, 2013
Clouds FM yakanusha KUHUSU MWANA FA
KUAHIRISHA SHOW YAKE YA THE FINEST LEO HII.Baada ya mtandao Feki wa
facebook utumiao jina lake kuandika kuwa show hiyo imeahirishwa.
Chanzo cha habari Udakuespecially
Chanzo cha habari Udakuespecially
NGASSA kuikosa Ivory Coast.
KIKOSI cha Taifa Stars kitashuka dimbani keshokutwa Jumapili kuivaa
Ivory Coast katika mechi ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2014, lakini
habari ni kuwa kiungo mshambuliaji wa Stars, Mrisho Ngassa hataruhusiwa
kucheza kwa kuwa ana kadi mbili za njano.
Taarifa ambazo Championi Ijumaa imezipata kutoka ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), zimesema kuwa wamepokea ujumbe kutoka Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kuwa Ngassa ana kadi mbili za njano.
Taarifa hiyo imesema kuwa, kiungo huyo alipata kadi mbili za njano katika michezo miwili ya nyumbani na ugenini wakati Stars ikiumana na Morocco, ambapo mchezo wa kwanza uliopigwa Machi, Stars ilishinda mabao 3-1 kabla ya kupokea kichapo cha mabao 2-1 ugenini.
“Tumepokea ujumbe kutoka Caf juu ya Ngassa, ni taarifa mbaya hasa katika siku hizi mbili kwa sababu tunajua kocha alikuwa anajua atakuwa naye katika mchezo wa keshokutwa,” alisema kiongozi huyo wa TFF.
Aidha, straika wa Stars, Mbwana Samatta: “Ile ni timu tu (Ivory Coast) kama timu nyingine, sijaona sababu za kuiogopa au kuihofia, tuna asilimia kibao za kushinda ukizingatia tunacheza nyumbani, ” alisema Samatta.
Taarifa ambazo Championi Ijumaa imezipata kutoka ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), zimesema kuwa wamepokea ujumbe kutoka Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kuwa Ngassa ana kadi mbili za njano.
Taarifa hiyo imesema kuwa, kiungo huyo alipata kadi mbili za njano katika michezo miwili ya nyumbani na ugenini wakati Stars ikiumana na Morocco, ambapo mchezo wa kwanza uliopigwa Machi, Stars ilishinda mabao 3-1 kabla ya kupokea kichapo cha mabao 2-1 ugenini.
“Tumepokea ujumbe kutoka Caf juu ya Ngassa, ni taarifa mbaya hasa katika siku hizi mbili kwa sababu tunajua kocha alikuwa anajua atakuwa naye katika mchezo wa keshokutwa,” alisema kiongozi huyo wa TFF.
Aidha, straika wa Stars, Mbwana Samatta: “Ile ni timu tu (Ivory Coast) kama timu nyingine, sijaona sababu za kuiogopa au kuihofia, tuna asilimia kibao za kushinda ukizingatia tunacheza nyumbani, ” alisema Samatta.
Baba mzazi wa Langa aweka wazi chanzo cha kifo cha mwanae
Baba mzazi we Langa, Mangisemi Kileo ameeleza chanzo cha kifo cha mwanaye ambaye kimetokea jana katika Hospitali ya Muhimbili.Langa amefariki dunia jana katika hospitali ya Muhimbili baada ya kulazwa usiku wa kuamkia jana.
Imeelezwa Langa alifikishwa hospitalini hapo akiwa amezidiwa na moja kwa moja akafikishwa katika chumba cha watu mahututi.
Salehjembe
ilifika nyumbani kwao marehemu eneo la Mikocheni Regency dakika chache
baada ya taarifa za msiba na kuzungumza na baba yake mzazi, Mengiseni
Kileo.
Kileo alisema Langa alizidiwa ghafla juzi, wakamkibiza katika Hospitali ya Kairuki.
“Pale walituambia kwamba anasumbuliwa maralia kali pamoja na ugonjwa wa uti wa mgongo.
“Hivyo
tukalazimika kumkimbiza Muhimbili ambako alifikishwa katika chumba cha
watu matuhuti (ICU), leo ndiyo mauti yamemkuta,” alisema.
Kuhusiana na mazishi, Kileo alisema wanalazimika kumsubiri mkewe, Venus ambaye anatarajia kutua nchini kesho au keshokutwa.
“Mama yake yuko Marekani, hivyo tutamsubiri lakini tumeshazungumza naye.
“Sisi tutakaa leo kujadili suala hilo na wanafamilia na baadaye tutajua kila kitu,” alisema Kileo akionyesha utulivu.
Langa alikuwa akitamba na nyimbo yake mpya ya Rafiki wa Kweli iliyotengenezwa katika studio za Bongo Record chini ya P Funk.
Msanii
huyo alianza kutamba baada ya kushinda usakaji vipaji chini ya Coca Cola
na kuunda kundi la Wakilisha akiwa na Shaa au Sarah na Witness wakianza
na wimbo wao wa kwanza ‘Hoi’.
Kutunza AMANI ni jukumu la kila Mtanzania
Tanzania ni nchi ya pekee inayosifika kwa amani duniani na hii ni kutokana na nguvu kubwa iliyofanywa na baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere. Na kweli kwa enzi zake kulikuwa hakuna haja ya kujiuliza maswali juu ya amani yetu. Lakini kwanzia tumpoteze Mwasisi wetu amani yetu imekuwa ikiyumba yumba kila kukicha kwa sababu kumekuwa kukitokea matatizo na matukio ya uharifu kila kikicha na hiki ni kiashirio tosha cha kushuka kwa amani yetu.
Nawaasa watanzania wote waone kama kutunza amani ni jukumu la kila mtanzania na si Serikali pekee.
AFRICAN BARRICK GOLD WATOA MILION 10 KWA REDS MISS MARA
Ofisa kutoka kitengo cha Mawasiliano na
Mahusiano wa Barrick Gold Mining Fatuma Mssumi akimkabidhi Kaimu Ofisa Tawala
wa Mkoa wa Mara mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 10, ikiwa ni
sehemu ya udhamini wa kampuni hiyo kwenye mashindano la Redd’s Miss Mara
yatakayofanyika leo mjini Musoma.
Mahusiano wa Barrick Gold Mining Fatuma Mssumi akimkabidhi Kaimu Ofisa Tawala
wa Mkoa wa Mara mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 10, ikiwa ni
sehemu ya udhamini wa kampuni hiyo kwenye mashindano la Redd’s Miss Mara
yatakayofanyika leo mjini Musoma.
Baadhi ya washiriki wa shindano la Redd’s Miss
Mara 2013 wakiwa katika picha ya pamoja jana ikiwa ni siku moja kabla ya
warembo hao hawajapanda jukwaani kuwania taji hilo ambalo linashikiliwa na Miss
Tanzania namba mbili 2012. Shindano hilo linataraji kufanyika leo.
Mara 2013 wakiwa katika picha ya pamoja jana ikiwa ni siku moja kabla ya
warembo hao hawajapanda jukwaani kuwania taji hilo ambalo linashikiliwa na Miss
Tanzania namba mbili 2012. Shindano hilo linataraji kufanyika leo.
Baadhi ya washiriki wa Redd’s Miss Mara 2013 wakiwa wenye furaha.
Baadhi ya warembo wakiwa katika pozi
Baadhi ya washiriki wa shindano la Redd’s Miss
Mara 2013 wakitembea kwa pamoja leo ikiwa ni siku moja kabla ya
warembo hao hawajapanda jukwaani kuwania taji hilo ambalo linashikiliwa na Miss Tanzania namba mbili 2012. Shindano hilo linataraji kufanyika leo.
Mara 2013 wakitembea kwa pamoja leo ikiwa ni siku moja kabla ya
warembo hao hawajapanda jukwaani kuwania taji hilo ambalo linashikiliwa na Miss Tanzania namba mbili 2012. Shindano hilo linataraji kufanyika leo.
Huyu ndiye mtoto wa miaka 14 wa kitanzania anayetengeneza application za simu na kuwauzia nokia
Tuesday, June 11, 2013
Alvin Walter Makundi ni kijana mdogo wa Kitanzania anayeishi na wazazi wake nchini Singapore. Akiwa na umri wa miaka 14 na mwanafunzi wa kidato cha pili huko Singapore, tayari ameshatumbukiza jina lake katika orodha ya wataalamu wa application katika moja ya makampuni makubwa duniani ya kutengeneza simu za mkononi ya NOKIA, ambapo anatengeneza applications ambazo anazituma katika kampuni hiyo ambayo nayo bila hiana huitumia.
Polisi Afukuzwa Kazi kwa Kupiga picha za Uchi Magomeni
POLISI wa kike wa Kituo cha Magomeni, jijini Dar es Salaam aliyejulikana
kwa jina moja la Anisa, ametimuliwa kazi kwa madai ya kupiga picha ya
utupu iliyosambaa mitandaoni.
Chanzo makini ndani ya jeshi hilo kilisema Anisa alifukuzwa kazi wiki iliyopita baada ya kuhojiwa na mabosi wake wa makao makuu ya jeshi hilo na kukiri kuwa picha hiyo ni yake.
“Anisa aliitwa makao makuu, mabosi wakamuonesha picha yake akiwa mtupu kitandani, akakiri ni yeye. Alijitetea eti alifanya hivyo kwa sababu siku ya tukio alikuwa amelewa sana,” kilisema chanzo.
Chanzo kiliendelea kudai kwamba baada ya afande huyo mwenyeji wa Tanga kukiri, viongozi wa jeshi hilo walimwambia amekiuka kanuni na kulidhalilisha jeshi hilo hivyo hataendelea kuwa mtumishi.
Picha ya afande huyo imeenea mitandaoni na kwenye baadhi ya simu za mikononi za watu kitendo kulicholifanya jeshi hilo kufanya uchunguzi na kubaini kuwa ni yake.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina, Suleiman Kova alipoulizwa juzi alikiri kufukuzwa kwa askari huyo na kumtaka mwandishi wetu kufuatilia zaidi kwa Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Camilius Wambura ambaye naye alipoulizwa kuhusu tukio hilo alikiri.
‘‘Tunahitaji askari wenye maadili mema ndani ya jeshi letu, yule atakayefanya mambo bila kufuata kanuni na sheria hatua kali zitachukuliwa dhidi yake. Askari muda wote anatakiwa awe mfano bora kwa jamii,’’ alisema Afande Wambura.
Taarifa zaidi zinadai kwamba kwa sasa Anisa anaishi uraiani kama raia wa kawaida.
Chanzo makini ndani ya jeshi hilo kilisema Anisa alifukuzwa kazi wiki iliyopita baada ya kuhojiwa na mabosi wake wa makao makuu ya jeshi hilo na kukiri kuwa picha hiyo ni yake.
“Anisa aliitwa makao makuu, mabosi wakamuonesha picha yake akiwa mtupu kitandani, akakiri ni yeye. Alijitetea eti alifanya hivyo kwa sababu siku ya tukio alikuwa amelewa sana,” kilisema chanzo.
Chanzo kiliendelea kudai kwamba baada ya afande huyo mwenyeji wa Tanga kukiri, viongozi wa jeshi hilo walimwambia amekiuka kanuni na kulidhalilisha jeshi hilo hivyo hataendelea kuwa mtumishi.
Picha ya afande huyo imeenea mitandaoni na kwenye baadhi ya simu za mikononi za watu kitendo kulicholifanya jeshi hilo kufanya uchunguzi na kubaini kuwa ni yake.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina, Suleiman Kova alipoulizwa juzi alikiri kufukuzwa kwa askari huyo na kumtaka mwandishi wetu kufuatilia zaidi kwa Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Camilius Wambura ambaye naye alipoulizwa kuhusu tukio hilo alikiri.
‘‘Tunahitaji askari wenye maadili mema ndani ya jeshi letu, yule atakayefanya mambo bila kufuata kanuni na sheria hatua kali zitachukuliwa dhidi yake. Askari muda wote anatakiwa awe mfano bora kwa jamii,’’ alisema Afande Wambura.
Taarifa zaidi zinadai kwamba kwa sasa Anisa anaishi uraiani kama raia wa kawaida.
Blog Archive
-
▼
2013
(21)
-
▼
June
(7)
- CLOUDS FM YAKANUSHA KUHUSU MWANA FA KUAHIRISHA SHO...
- NGASSA kuikosa Ivory Coast.
- Baba mzazi wa Langa aweka wazi chanzo cha kifo ch...
- Kutunza AMANI ni jukumu la kila Mtanzania
- AFRICAN BARRICK GOLD WATOA MILION 10 KWA REDS MISS...
- Huyu ndiye mtoto wa miaka 14 wa kitanzania anayete...
- Polisi Afukuzwa Kazi kwa Kupiga picha za Uchi Mago...
-
▼
June
(7)
Followers
Blog Archive
-
▼
2013
(21)
-
▼
June
(7)
- CLOUDS FM YAKANUSHA KUHUSU MWANA FA KUAHIRISHA SHO...
- NGASSA kuikosa Ivory Coast.
- Baba mzazi wa Langa aweka wazi chanzo cha kifo ch...
- Kutunza AMANI ni jukumu la kila Mtanzania
- AFRICAN BARRICK GOLD WATOA MILION 10 KWA REDS MISS...
- Huyu ndiye mtoto wa miaka 14 wa kitanzania anayete...
- Polisi Afukuzwa Kazi kwa Kupiga picha za Uchi Mago...
-
▼
June
(7)