S.L.P …., Musoma-Mara. Simu: 0756290672, 0755671818, & 0654655498
VIJANA MANISPAA YA MUSOMA KUAZIMIA KUUNDA CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPO
Monday, April 14, 2014
CHAMA CHA USHIRIKA
CHA AKIBA NA MIKOPO CHA VIJANA MUSOMA SACCOS (VIMU SACCOS) LTD
S.L.P …., Musoma-Mara. Simu: 0756290672, 0755671818, & 0654655498
S.L.P …., Musoma-Mara. Simu: 0756290672, 0755671818, & 0654655498
Vijana wapatao 45, manispaa ya
Musoma wameazimia kuunda na kusajiri Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo
kijulikanacho kwa jina la VIJANA MUSOMA SACCOS LTD kwa lengo la kuinuana khali
zao kiuchumi na kijamii.
Mwenyekiti wa Bodi ya uanzilishi
wa Chama hicho, Bwn. Japheth M. Kurwa; alisema “Wanachama wa chama cha ushirika
cha VIJANA MUSOMA SACCOS (VIMU SACCOS) tumeamua rasmi na kwa dhati
kusaidiana, kushirikiana, kuthaminiana, kujaliana, kujiendeleza na kusimamia
ubora wa maisha yetu ili kila mmoja apate unafuu na furaha katika maisha kwa
kuzingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani, Madhumuni ya chama hiki
cha ushirika ni kuinua na kuimarisha hali ya kiuchumi na kijamii ya wanachama
wake (Vijana) kwa kufuata kanuni na taratibu za vyama vya ushirika. Hivyo basi napenda kutoa wito kwa vijana wote
wa manispaa ya Musoma kujiunga na Chama hiki. Vijana Musoma SACCOS ni
kwa Ajiri ya Maendeleo yako Binafsi, Familia yako, Jamii yako, na Taifa kwa Ujumla”.
“Weka Akiba
Mara kwa Mara, Kopa kwa Busara, Lipa Upesi”
MAUAJI YA KIKATILI DHIDI YA WANAWAKE KUENDELEA MKOANI MARA
Kulia juu ni picha ya mwili wa marehemu Nyamata Gwanumbu Monda Nyamsha, na ya pili ni maafisa wa polisi wakishusha mwili wa mareheu nyumbani kwao Kiemba Nyakatende.
Mama mmoja aliyefahamika kwa
majina ya Nyamata Gwanumbu Monda Nyamsha, mwenye umri wa miaka iliyokadiriwa
38, watoto 5. Mkazi wa Mkoa: Mara, Wilaya: Butiama, Kata: Nyakatende, Kijiji:
Kiemba. Tarehe 10 April, 2014 Saa 3
Asubuhi alikutwa shambani kwake akiwa mauti na amezikwa kwa kufukiwa kwa udongo
chini ya kichaka kilichoko shambani kwake, hata hivyo marehemu alikutwa ana
jereha la kupigwa kichwani eneo la kisogoni.
Kisa Mkasa
Marehemu asubuhi aliwahi kuamka
na kuelekea shambani kwake kuchimba viazi huku akiwa amewaachia watoto wake
maagizo ya kuja saa 3 asubuhi shambani hapo kumpokea viazi atakavyokuwa
amechimba. Mda huo ulipofika watoto wa marehemu walikwenda shambani kufuata
viazi kama marehemu mama yao alivyokuwa amewaambia. Walipofika shambani hawakumuona marehemu mama
yao ndipo walianza kuita mama mama……, ghafla walimuona mtu (mwanamume) akitoka
kichakani akiwa uchi kama alivyozaliwa akiwa na panga mkononi, walikimbia
wakipiga kelele. Ndipo wananchi
walipojitokeza kujua kulikoni. Katika zoezi la kumtafuta mama huyo ndipo
alipokutwa kichakani hapo akiwa ameuwawa.
Kwa mujibu wa Mhe. Diwani wa kata
ya Nyakatende Ndg.Kasonyi mauaji hayo ni mauaji ya nne(4) tangu mauaji hayo
yaanze kuzuka wilani Butiama, Mugango mauaji mara mbili (2), yakiongozwa na
Nyegina mauaji mara nane (8)
Tarehe 22/03/2014 saa 2 Asubuhi
yalitokea mauaji mengine pia ya mama aliyefahamika kwa majina ya Yasinta
Kate Matiku kwa kabila Mkwaya, miaka 34, na familiya ya watoto 2. Mkazi wa
Kijiji cha Kamguruki, Kata ya Nyakatende, Tarafa ya Nyanja, Wilaya ya Butiama,
mkoani Mara.
Kisa Mkasa
Asubuhi ya saa 2 marehemu
aliondoka nyumbani kwenda kununua vitumbua gengeni(Center), ndiko alipokutwa na
mauaji hayo. Mwili wake ulikuwa unajeraha kupigwa na kitu chenye incha kali,
kisha kumwagiwa maji ya moto sehemu za mapajani, mgongoni na mbavuni, mkanda wa
suruali shingoni na ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo vyake vya siri (maalufu
kwa jina la Memory card)
Ukiwa mzalendo na mpenda Amani
unashauri nini kifanyike………………………….?, Toa maoni yako ili kutokomeza mauaji haya
yanayoendelea.