Karibu Musoma Information Center kwa huduma zifuatazo:- 1) Kwa kutengenezewa design mbalimbali kama za Business card, Vipeperushi, mabango mbalimbali, kadi za Harusi za kisasa zaidi, kadi za mialiko mbalimbali, Vitambulisho vya wanafunzi wa sekondari na katika kampuni mbalimbali ( ID cards) na kadi nyinginezo zenye design ya kuvutia. 2) Kutengenezewa mabango ( Posters) mbalimbali zinazohusu biashara ya mhusika au bidhaa mbalimbali. 3) Kutengenezewa nembo ( LOGO) za kuhusiana kampuni au biashara yako. 4) Tunatengeneza tovuti ( Websites ) zenye kiwango ambacho huwezi amini kama zinatengenezwa musoma, kwa bei nafuu ambayo huwezi ipata kwingine isipo kuwa kwetu. 5) Mwisho tunatoa ushauri na elimu kuhusiana na maswala ya computer.5) Sisi ni watengenezaji wa blog zinazokaa mfumo wa website. kama hii unayoiona.

Welcome to TYPS - ASSOCIATION

Welcome to TYPS - ASSOCIATION

Welcome

A Letter from the Executive Director

Dear All,

As Executive Director it is my pressure to welcome you to TANZANIA YOUTH POTENTIALS ASSOCIATION (TYPs-ASSOCIATION)-a growing youth-led Organization with it’s headquarter in Musoma that operates through legal registration number 00NGO/00006304 under the ACT of 2002 in Tanzania. The focus of the organization is to utilize youth’s potentials for their own development, community and state development at large. It also intends to strengthen regional and international interventions towards protection and promotion of the human rights especially to children, youth and women. It works with networking with other partners/ stakeholders and beneficiaries.

The Organization has the mission of striving and inheriting youth and other community groups with various technical capacities eligible to make them be engines for socio-economic growth for individual benefits, societies and the national at large as such to see a community in which women’s and children’s rights are observed and respected by executing mobilization projects eligible to bring positive changes to community through action and participation in collaboration with community and other stakeholders to prevent Gender Based Violence (GBV).

However the organization is dedicated to develop dynamic and entrepreneurial youths who will engage and realize their full potential and that of their community, their country and the world at large and advocating The National Youth Development Policy

The Secretariat , the Board of Directors and the Annual General Meeting of TYPs-ASSOCIATION eagerly anticipate your arrival and contribution to its future, and welcome you to discover youth development experience that promotes your Personal and intellectual growth

Welcome to TYPs-ASSOCIATION,
Mr. Japheth M. Kurwa
Executive Director


VIJANA MANISPAA YA MUSOMA KUAZIMIA KUUNDA CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPO

Monday, April 14, 2014





CHAMA CHA USHIRIKA CHA AKIBA NA MIKOPO CHA VIJANA MUSOMA SACCOS (VIMU SACCOS) LTD
S.L.P …., Musoma-Mara. Simu: 0756290672, 0755671818, & 0654655498

Vijana wapatao 45, manispaa ya Musoma wameazimia kuunda na kusajiri Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo kijulikanacho kwa jina la VIJANA MUSOMA SACCOS LTD kwa lengo la kuinuana khali zao kiuchumi na kijamii.
Mwenyekiti wa Bodi ya uanzilishi wa Chama hicho, Bwn. Japheth M. Kurwa; alisema “Wanachama wa chama cha ushirika cha VIJANA MUSOMA SACCOS (VIMU SACCOS) tumeamua rasmi na kwa dhati kusaidiana, kushirikiana, kuthaminiana, kujaliana, kujiendeleza na kusimamia ubora wa maisha yetu ili kila mmoja apate unafuu na furaha katika maisha kwa kuzingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani, Madhumuni ya chama hiki cha ushirika ni kuinua na kuimarisha hali ya kiuchumi na kijamii ya wanachama wake (Vijana) kwa kufuata kanuni na taratibu za vyama vya ushirika. Hivyo basi napenda kutoa wito kwa vijana wote wa manispaa ya Musoma kujiunga na Chama hiki. Vijana Musoma SACCOS ni kwa Ajiri ya Maendeleo yako Binafsi, Familia yako, Jamii yako, na Taifa kwa Ujumla.
“Weka Akiba Mara kwa Mara, Kopa kwa Busara, Lipa Upesi”

MAUAJI YA KIKATILI DHIDI YA WANAWAKE KUENDELEA MKOANI MARA



Kulia juu ni picha ya mwili wa marehemu Nyamata Gwanumbu Monda Nyamsha, na ya pili ni maafisa wa polisi wakishusha mwili wa mareheu nyumbani kwao Kiemba Nyakatende.

Mama mmoja aliyefahamika kwa majina ya Nyamata Gwanumbu Monda Nyamsha, mwenye umri wa miaka iliyokadiriwa 38, watoto 5. Mkazi wa Mkoa: Mara, Wilaya: Butiama, Kata: Nyakatende, Kijiji: Kiemba. Tarehe 10 April, 2014 Saa 3 Asubuhi alikutwa shambani kwake akiwa mauti na amezikwa kwa kufukiwa kwa udongo chini ya kichaka kilichoko shambani kwake, hata hivyo marehemu alikutwa ana jereha la kupigwa kichwani eneo la kisogoni.


Kisa Mkasa
Marehemu asubuhi aliwahi kuamka na kuelekea shambani kwake kuchimba viazi huku akiwa amewaachia watoto wake maagizo ya kuja saa 3 asubuhi shambani hapo kumpokea viazi atakavyokuwa amechimba. Mda huo ulipofika watoto wa marehemu walikwenda shambani kufuata viazi kama marehemu mama yao alivyokuwa amewaambia.  Walipofika shambani hawakumuona marehemu mama yao ndipo walianza kuita mama mama……, ghafla walimuona mtu (mwanamume) akitoka kichakani akiwa uchi kama alivyozaliwa akiwa na panga mkononi, walikimbia wakipiga kelele.  Ndipo wananchi walipojitokeza kujua kulikoni. Katika zoezi la kumtafuta mama huyo ndipo alipokutwa kichakani hapo akiwa ameuwawa.
Kwa mujibu wa Mhe. Diwani wa kata ya Nyakatende Ndg.Kasonyi mauaji hayo ni mauaji ya nne(4) tangu mauaji hayo yaanze kuzuka wilani Butiama, Mugango mauaji mara mbili (2), yakiongozwa na Nyegina mauaji mara nane (8)

Tarehe 22/03/2014 saa 2 Asubuhi  yalitokea mauaji mengine pia ya mama aliyefahamika kwa majina ya Yasinta Kate Matiku kwa kabila Mkwaya, miaka 34, na familiya ya watoto 2. Mkazi wa Kijiji cha Kamguruki, Kata ya Nyakatende, Tarafa ya Nyanja, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara.

Kisa Mkasa
Asubuhi ya saa 2 marehemu aliondoka nyumbani kwenda kununua vitumbua gengeni(Center), ndiko alipokutwa na mauaji hayo. Mwili wake ulikuwa unajeraha kupigwa na kitu chenye incha kali, kisha kumwagiwa maji ya moto sehemu za mapajani, mgongoni na mbavuni, mkanda wa suruali shingoni na ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo vyake vya siri (maalufu kwa jina la Memory card)
Ukiwa mzalendo na mpenda Amani unashauri nini kifanyike………………………….?, Toa maoni yako ili kutokomeza mauaji haya yanayoendelea.

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. TZ Youth Potentials - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Inspired by Sportapolis Shape5.com
Proudly powered by Blogger